Katika kozi ya Bachelor in Optometry, mwanafunzi hujifunza masomo muhimu yanayohusiana na afya ya macho. Haya ni pamoja na Anatomy na Physiology ya jicho, ili kuelewa mfumo wa macho unavyofanya kazi; Optics, kuhusu jinsi mwanga unavyoingia machoni na namna ya kurekebisha matatizo ya kuona; na Clinical Optometry, inayohusisha mbinu za kupima macho kitaalamu. Vilevile, wanafunzi hufundishwa kutumia Ophthalmic Instruments za kisasa kwa ajili ya upimaji wa macho, kushughulika na Contact Lenses & Low Vision Aids kusaidia wenye uoni hafifu, na pia kujifunza kuhusu Ocular Diseases, magonjwa ya macho na mbinu za kuyatibu.
Fursa za ajira kwa mhitimu wa Optometry ni nyingi na pana. Wanaweza kufanya kazi katika hospitali kubwa za macho kama CCBRT, Muhimbili, Aga Khan na KCMC, au kwenye clinics binafsi za macho. Aidha, mhitimu anaweza kuanzisha au kufanya kazi katika optical shops zinazouza miwani na kutoa huduma za kupima macho. Kwa wale wanaopenda taaluma ya utafiti na elimu, kuna nafasi katika vyuo vikuu na taasisi za utafiti wa macho. Pia, mashirika ya afya ya macho ya kimataifa kama Sightsavers, Fred Hollows Foundation na Vision 2020 huwapa nafasi kubwa ya ajira Optometrists.
Kwa upande wa kujiajiri, mhitimu wa Optometry anaweza kufungua optical shop au clinic ndogo ya macho, kutoa huduma za mobile eye clinic hasa vijijini ambako upatikanaji wa huduma hizi ni mdogo, au hata kuanzisha biashara ya miwani na lensi.
Kwa sasa, Tanzania ina Diploma ya Optometry pekee, na bado hakuna shahada ya kwanza. Hii ina maana kwamba wanaosoma Bachelor in Optometry nje ya nchi, hususan India, wanapokuwa wamemaliza masomo hupata nafasi kubwa zaidi ya ajira, nafasi za uongozi katika mashirika na hospitali za macho, na hata heshima ya kitaalamu zaidi katika soko la ajira.
Kozi hii ni ya maana sana kwa sababu wagonjwa wa macho nchini Tanzania na Afrika Mashariki ni wengi sana huku wataalamu wakiwa wachache. Pia, ni taaluma inayochanganya afya na biashara, kwa kuwa mhitimu anaweza kuwa mtaalamu wa macho na wakati huohuo kuwa mfanyabiashara wa opticals. Kwa kuwa hakuna shahada ya Optometry nchini Tanzania, mhitimu wa ngazi hii anakuwa na faida kubwa kwenye soko la ajira.
Kutoka/Kupitia Akili Education
