Chuo cha Ualimu Mhonda kipo katika Mkoa wa Morogoro, Wilaya ya Mvomero, Tarafa ya Turiani, Kata ya Mhonda, Kijiji cha Mhonda. Ni umbali wa kilometa 104 kutoka Stendi ya Msamvu iliyopo Morogoro mjini, na kilometa 3½ kutoka Turiani kituo cha mabasi Mapate hadi Chuoni.
MOTTO WA CHUO
“ELIMU ILETE USAWA WA BINADAMU”
MASOMO YANAYOFUNDISHWA
(i) Chuo kinaendesha Mafunzo ya(i) Stashahada ya Ualimu Elimu ya Msingi Mchepuo wa Sayansi ya Jamii kwa kutumia lughaya Kiswahili kwa muda wa miaka mitatu (3).
(ii) Stashahada ya Ualimu Elimu ya Awali kwa kutumia lugha ya Kiswahili kwa muda wa miakamitatu (3).
DIRA YA CHUO
Kuandaa Walimu Walio Bora, Wazalendo, Wenye Maadili, Wanaojali Jinsia, Haki na Wajibu, KwaKutumia Miundo Mbinu Thabiti Kwa Kuzingatia Mahitaji ya Jamii na Taifa”(c)
DHAMIRA YA CHUO
“Chuo kuwa Chachu ya Mabadiliko Chanya Kitaaluma, Kitaalam na Kimaadili kwa KuchocheaUbunifu, Udadisi, Utafiti na Kuthubutu Kutenda ili Kuiwezesha Jamii Kukabiliana na ChangamotoZitokanazo na Mabadiliko ya Sayansi na Teknolojia katika Kuleta Mabadiliko Endelevu”










