Home JESHI LA POLISI Tangazo la kuitwa mafunzo jeshi la polisi tanzania 2025

Tangazo la kuitwa mafunzo jeshi la polisi tanzania 2025

426
0

TANGAZO LA KURIPOTI SHULE YA POLISI MOSHI KWA

VIJANA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA JESHI LA POLISI

TANZANIA

1. Mkuu wa Jeshi la Polisi anawatangazia vijana waliochaguliwa kujiunga na

Jeshi la Polisi Tanzania kuwa wanatakiwa kuripoti Shule ya Polisi Moshi

kuanzia tarehe 12/06/2025 hadi tarehe 14/06/2025 kwa ajili ya kuhudhuria

mafunzo.

2. Vijana waliofanyiwa usaili Dar es Salaam kwenye Vikosi vilivyo chini ya

Makao Makuu ya Polisi wataripoti jijini Dar es Salaam katika uwanja

wa gwaride uliopo Kambi ya Polisi (Police Barracks) barabara ya

Kilwa nyuma ya kituo cha Polisi Kilwa Road tarehe 12/06/2025 saa

12.00 asubuhi kwa ajili ya safari ya kwenda Shule ya Polisi Moshi.

3. Vijana waliofanyiwa usaili Mikoa ya Tanzania Bara wanatakiwa kuripoti

kwa Makamanda wa Polisi wa Mikoa waliofanyia usaili tarehe 11/06/2025

saa 2.00 asubuhi kwa ajili ya kupewa utaratibu wa safari ya kwenda Shule

ya Polisi Moshi.

4. Vilevile, vijana waliofanyia usaili Zanzibar (Unguja na Pemba)

wanatakiwa waripoti Makao Makuu ya Polisi Zanzibar (Ziwani) tarehe

11/06/2025 saa 2.00 asubuhi kwa ajili ya kupangiwa utaratibu wa safari.

5. Aidha, vijana wote waliochaguliwa wanatakiwa kuripoti Shule ya Polisi

Moshi wakiwa na vifaa vifuatavyo:

i) Traki suti (track suit) rangi ya bluu (blue) yenye ufito mweupe, fulana

(t-shirt) nyeupe isiyo na maandishi, raba, soksi nyeusi, bukta mbili

(2) za bluu (blue) kwa ajili ya michezo na mazoezi pamoja na

sanduku la chuma (Tranka) la rangi ya bluu.

ii) Chandarua cheupe cha duara na sio cha pembe nne, shuka za rangi ya

bluu mpauko (light blue) jozi mbili (Shuka 4), pasi ya mkaa na

blanket moja la kijivu lisilo na maua na sio duveti.

iii) Kikombe cha plastiki ambacho kimetengenezwa kwa matirio ya

mfupa (Cream light), Sahani moja aina ya ‘steel dish plate’.

iv) Vifaa vya usafi: Sururu moja lenye mpini, ndoo mbili ndogo na fagio

la chelewa.

v) Kadi ya bima ya Afya (NHIF) kama anayo au fedha taslimu Tsh.

50,400/= kwa wasio na kadi za bima ya Afya.

vi) Vyeti halisi vya taaluma (Original Academic Certificates), cheti

halisi cha kuzaliwa, kadi ya NIDA au namba ya Utambulisho wa

Taifa (NIDA), Nakala za kadi za NIDA au namba za Utambulisho wa

Taifa (NIDA) za wazazi na watu wa karibu upande wa Baba na Mama

(kama vile Baba, Baba mkubwa, Baba mdogo, Shangazi, Mama,

Mama mkubwa, Mama mdogo, Mjomba, Babu nk), passport size 6

(background blue), na nakala (copy) 5 kwa kila cheti kilichoainishwa

hapo juu.

vii) Fedha za kujikimu.

PAKUA MAJINA HAPA PDF YA MAJINA

 

6. Simu za mkononi haziruhusiwi chuoni, hivyo ni marufuku kuripoti Shule

ya Polisi Moshi ukiwa na simu ya mkononi. Yeyote atakayepatikana na

simu itachukuliwa kuwa ni utovu wa nidhamu na adhabu yake ni

kufukuzwa mafunzo mara moja. Shule itaelekeza utaratibu wa kupata

mawasiliano.

7. Kwa yeyote atakayeripoti Shule ya Polisi Moshi baada ya tarehe

14/06/2025 hatopokelewa na atahesabika amejiondoa mwenyewe kwenye

mafunzo.

8. Orodha ya vijana waliochaguliwa imeambatishwa kwenye tangazo hili.

Imetolewa na;

Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania,

Makao Makuu ya Jeshi la Polisi,

S.L.P 961,

DODOMA.

01/06/2025.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here