Home NECTA Jinsi Ya Kupata Cheti Mbadala NECTA Form Four/Six Kama Umepoteza

Jinsi Ya Kupata Cheti Mbadala NECTA Form Four/Six Kama Umepoteza

25
0
📢 JIUNGE NA CHANNEL YETU

Fahamu Jinsi Ya Kupata Cheti Mbadala NECTA CSEE/ACSEE Umepoteza.

Hakikisha kwamba unavyo viambatisho vifuatavyo :-

lwapo cheti kimepotea, tangazo la gazeti la upotevu wa cheti (taarifa muhimu kwenye tangazo hilo ni Jina la mtahiniwa, Namba ya mtihani, aina ya mtihani, mwaka wa mtihani, jina la shule, picha ya mtahiniwa na mahali cheti kilikopotea), Hati ya polisi ya upotevu wa cheti, Picha (Passport size) utakayobandika kwenye fomu ya ombi la cheti mbadala, Nakala ya kitambulisho na Risiti halisi ya malipo au “Control Number”.

lwapo cheti chako kiliungua moto, kuharibiwa na mchwa, mafuriko, panya au kwa namna nyingine yoyote hutatakiwa kutangaza gazetini juu ya uharibifu huo bali utawasilisha vielelezo vilivyotajwa hapo juu pamoja na barua ya serikali ya mtaa wa eneo la tukio la moto au mafuriko yalipotokea. Iwapo yapo mabaki ya cheti husika utatakiwa kuwasilisha mabaki hayo Baraza la Mitihani la Tanzania.

Baada ya kukamilisha ujazaji wa fomu na malipo, tafadhali tuma au wasilisha fomu yenye viambatisho vilivyotajwa kwa Katibu Mtendaji, Baraza la Mitihani la Tanzania, S.L.P 2624, Dar es Salaam.

Malipo kwa ajili ya huduma ya cheti mbadala yafanyike kwa kutumia namba maalum (Control Number) inayotolewa na mfumo wa malipo ya serikali wa kielektroniki (GePG) kupitia tovuti ya NECTA: www.necta.go.tz au piga simu namba +255-22-2700493 … 6 kwa msaada zaidi.

Malipo yote yafanyike katika benki za: NMB; CRDB na NBC au kwa kutumia mitandao ya kifedha ya M-Pesa na Tigo Pesa.

MASHARTI YA KUOMBA CHETI MBADALA

Mwombaji wa cheti mbadala unatakiwa kutimiza masharti yafuatayo :-

(a) Uwe ni mtahiniwa halisi uliyefanya mtihani na kutunukiwa cheti cha awali chenye picha kisha kikapotea, kuharibika au kuungua moto.

(b) Uwe mkweli, mwaminifu na mwenye dhamira ya kweli ya hitaji la cheti mbadala baada ya kutokuwa na cheti cha awali kwa sababu ya matukio yaliyotajwa katika kipengele (a) hapo juu.

(c) Picha yako itafananishwa na picha iliyotumika kufanya mtihani husika. Iwapo picha hizo hazitafanana, uchunguzi utafanyika ili kubaini ukweli wa tofauti hizo. Aidha, iwapo matokeo ya uchunguzi yatabaini kuwa aliyefanya mtihani huo ni mtahiniwa tofauti na wewe, basi itakuwa imethibitika kuwa ulikuwa unajaribu kujipatia cheti mbadala isivyo halali kinyume cha sheria.

Hivyo, hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yako.

(d) Cheti mbadala kitatumiwa na mtahiniwa husika tu katika ajira na mafunzo. Iwapo cheti

kilichopotea (kwa waliopoteza vyeti) kitapatikana, cheti mbadala kirudishwe Baraza la Mitihani mara moja.

(e) Uwe umetekeleza maelekezo yote yaliyoainishwa katika vipengele (a) hadi (d) hapo juu.

Nyaraka Zinazohitajika Wakati wa Maombi

a) Ripoti ya Upotevu wa Polisi au Ripoti ya Maafa ya Moto / Mafuriko.

b) Ukurasa mzima wa gazeti lenye notisi ya upotevu inayoonyesha jina la mtahiniwa, nambari ya mtihani, aina ya mtihani, mwaka wa mtihani, jina la shule, picha ya mtahiniwa na mahali ambapocheti kilipotea) au;

c) Barua kutoka kwa Jeshi la Uokoaji wa Moto au serikali ya mtaa kuhusu kuungua au uharibifu wacheti kilichosababishwa na mafuriko, sisimizi, panya au uharibifu mwingine wowote.

d) Mabaki ya cheti (ikiwa kipo) baada ya kuharibiwa na mafuriko, ajali ya moto au panya nasisimizi.

e) Nakala ya mojawapo ya vitambulisho vifuatavyo: Kitambulisho cha Mpiga Kura, Kitambulisho cha Taifa, Leseni ya Udereva au Pasipoti. Vitambulisho vingine havitakubaliwa.

f) Picha ya ukubwa wa pasipoti yenye rangi yenye mandhari ya bluu.

g) Lipa Tshs. 100,000/= kwa kila cheti kilichopotea katika moja ya Benki zifuatazo. NMB, CRDB, NBCau kupitia mfumo wa malipo wa simu ya mkononi k.m. M – Pesa au Tigo-Pesa kwa kutumia control namba uliyounda.

h) Mwombaji ambaye amepoteza Cheti chake cha Kubadilisha, anapaswa kulipa Sh. 150,000 ili apewe Cheti kingine cha Kubadilisha.

i) Cheti cha Kubadilisha/Kurudia kitatumwa kwa anwani ya posta ya mwombaji (kwa ombi) au kitachukuliwa kimwili kutoka ofisi ya NECTA (Makao Makuu) SI chini ya siku thelathini (30) za kazi kuanzia tarehe ya kuwasilisha maombi.

 

📢 JIUNGE NA CHANNEL YETU

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here