TAARIFA KWA UMMA – DIRISHA LA UOMBAJI MIKOPO 2026/2027
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU ZANZIBAR (BMWEJZ / ZHESLB)
Tarehe: 03 Julai, 2026
DIRISHA LA UOMBAJI MIKOPO LIMEFUNGULIWA
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu Zanzibar inawataarifu umma kuwa Dirisha la maombi ya mikopo kwa mwaka wa masomo 2026/2027 limefunguliwa rasmi.
VIWANGO VYA MASOMO YANAYOKUBALIWA
Maombi yanakubalika kwa viwango vifuatavyo:
- Diploma
- Digrii (Degree)
- Masters
- PhD
TAREHE MUHIMU
| Aina ya Maombi | Tarehe ya Kufungua | Tarehe ya Kufunga |
| Mikopo ya Ndani ya Nchi (Tanzania) | 03 Julai, 2026 | 31 Agosti, 2026 |
| Mikopo ya Nje ya Nchi (Abroad) | 03 Julai, 2026 | 31 Julai, 2026 |
MAELEKEZO KWA WAOMBAJI
- Soma Muongozo Vizuri – Waombaji wote wanaombwa kusoma vizuri muongozo wa uombaji mikopo unaopatikana kwenye tovuti rasmi ya Bodi.
- Tovuti Rasmi:Â www.zheslb.go.tz
- Jinsi ya Kuwasilisha Maombi: Maombi yote yawasilishwe kwa njia ya mtandao kupitia mfumo wa ZOLAS (ZHESLB Online Loans Application System).
- Kiunganishi (Link) cha Kuwasilisha Maombi:
https://zolas.zheslb.go.tz/zolas
MUHIMU KUKUMBUKA
- Hakikisha umeomba ndani ya muda uliopangwa.
- Maombi yaliyowasilishwa baada ya tarehe ya mwisho hayatakubaliwa.
- Fuata taratibu zote zilizoainishwa kwenye muongozo wa uombaji mikopo.
- Hakikisha umesoma na kuelewa muongozo kabla ya kuanza mchakato wa kuomba.
WITO KWA WAOMBAJI
Bodi inawahimiza waombaji wote kuchukua fursa hii na kuwasilisha maombi yao mapema ili kuepuka msongamano wa dakika za mwisho.
Imetolewa na:
Kitengo cha Habari, Taaluma na Uhusiano
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu Zanzibar
“LIPA MKOPO NA WENGINE WASOME”
© 2026 Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu Zanzibar. Haki zote zimehifadhiwa.









